Home Makala Azam Fc Yailaza Singida Stars

Azam Fc Yailaza Singida Stars

by Sports Leo
0 comments

Singida Big Stars imekubali kipigo cha 1-0 kutoka kwa Azam Fc katika mchezo wa ligin kuu uliofanyika katika uwanja wa Azam Complex ulioko Chamazi jijini Dar es salaam bao likifungwa na Sospeter Bajana mapema dakika ya 45 za kipindi cha kwanza.

Azam Fc licha ya kuwa na matokeo mabaya katika mchezo wake dhidi ya Tanzania Prisons Fc ilifanikiwa kuonyesha mchezo mzuri na wenye mipango kiasi cha kupata matokeo katikamchezo huo wakiwabana Singida Stars katika kipindi chote cha mchezo huo na mpaka mpira unamalizika Azam Fc iliondoka na alama tatu katika mchezo huo uliowavutia wadau wengi wa soka hapa nchini.

Azam Fc kutokana na ushindi hu sasa imefikisha alama 11 katika nafasi ya sita ikicheza jumla ya michezo sita ya ligi kuu nchini huku Simba sc na Yanga sc zikiwa kileleni japo zina mchezo mmoja mkononi.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited