Klabu ya Azam Fc imeamua kuachana na kocha wake wa timu ya wakubwa Abdihamid Moallin pamoja na msaidizi wake Omary Nasser ambao wameachia ngazi kama kocha mkuu na msaidizi huku wakisubiri kupangiwa majukumu mengine ya kiufundi.
Maamuzi hayo yamefikiwa mapema kutokana na kutoridhishwa na mwenendo wa timu katika michezo miwili ya ligi kuu waliyocheza mpaka sasa ambapo katika michezo miwili wamefanikiwa kupata alama nne kati ya sita wakiwafunga Kagera Sugar 2-1 na kupaa sare dhidi ya Geita Gold ya 1-1.
Inasemekana kuwa mabosi wa klabu hiyo hawaridhishwi na ubora wa kikosi hicho ambapo wanaona kuwa kiwango cha timu kipo chini ukilinganisha na usajili waliofanya hivyo wanaona kama kocha hatoshi katika nafasi hiyo hivyo wanatafuta kocha mzoefu zaidi.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.