Klabu ya Azam Fc imeamua kuachana na wachezaji wake wawili kipa Ahmed Salula na mshambuliaji Shabani Idd Chilunda kwa makubaliano ya pande mbili baada ya kushindwa kulishawishi benchi la ufundi la klabu hiyo yenye maskani yake Chamazi jijini Dar es salaam.
Azam Fc imefanya usajili mkubwa katika dirisha kubwa la usajili lililopita na mpaka sasa katika dirisha hilo dogo la usajili imeendelea kufanya marekebisho kadhaa ya kikosi huku tayari mbali ya kuachana na mastaa hawa tayari imeshaachana na Ibrahim Ajibu ambaye ilimsajili baada ya kuachana na Simba sc.
Katika msimamo wa ligi kuu nchini msimu huu Azam Fc ipo nafasi ya tatu ikiwa na alama 37 katika michezo 18 ya ligi kuu ikizidiwa alama kumi na vinara Yanga sc.