Home Makala Azam Wakwama Kwa Dodoma Jiji

Azam Wakwama Kwa Dodoma Jiji

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Azam Fc imelazimishwa suluhu na klabu ya Dodoma Jiji Fc katika mchezo wa ligi kuu nchini uliofanyika usiku huu katika uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma.

Azam Fc ikimkosa mshambuliaje wake mahiri Prince Dube ilimuanzisha mshambuliaji mwenye mwili mkubwa Allasane Diara aliyesaidiwa na Feisal Salum,Gibri Sylla na viungo wakabaji Sospeter Bajana na Yannick Bangala walishindwa kuizidi maarifa safu ya kiungo ya Dodoma Jiji iliyoongozwa na Mtenje Albano pamoja na Gustavo Saimoni.

Kipindi cha kwanza kilimalizika kwa suluhu huku kipindi cha pili licha ya jitihada za walime Melis Medo na Yousouph Dabo kufanya mabadiliko bado hayakuzaa matunda na kusababisha mpaka dakika tisini kumalizika kwa matokeo hayo.

banner

Kutokana na hilo sasa Azam Fc imefikisha alama 10 katika michezo minne ya ligi kuu ikishinda mitatu na suluhu moja huku Dodoma Jiji ikifikisha alama 5 katika michezo minne ya ligi kuu ya Nbc nchini.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited