Home Makala Azam Yapania Ubingwa Ligi Kuu Bara

Azam Yapania Ubingwa Ligi Kuu Bara

by Sports Leo
0 comments

Azam Fc iliyo chini ya kocha mkuu,Aristica Ciaoba imepania kuupata ubingwa wa ligi kuu bara msimu huu wa 2020/2021 baada ya kujua mapungufu yao yapo wapi na kuyafanyia marekebisho.

Klabu hiyo iliyo na makazi yake chamazi inaongoza kwa sasa katika msimamo wa ligi kuu bara baada ya kucheza mechi nne huku ikishinda michezo yote na kujikusanyia pointi 12.

Azam imewaacha nyuma wapinzani wao Simba Sc na Yanga Sc kwa pointi mbili ambapo kwa sasa wameamua pia kuwaundia mikakati mizito timu hizo ili iendelee kushika usukani wa ligi na kuhakikisha wananyakuwa pointi tatu katika kila mechi.

banner

Octoba 4,Jumapili Azam itakabiliana na Kagera Sugar katika raundi ya tano ya ligi kuu bara majira ya saa1:00 kwenye uwanja wao wa Azam Complex.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited