Home Makala Balinya Atua Gormahia

Balinya Atua Gormahia

by Sports Leo
0 comments

Aliyekuwa mshambuliaji wa Yanga Juma Balinya amesajiliwa na timu ya Gor Mahia, mabingwa wa ligi kuu ya Kenya.

Gor Mahia imemsajili Balinya baada ya kujiridhisha na uwezo wake hasa baada ya kuwa mfungaji bora wa ligi kuu ya Uganda kwa msimu uliopita.

Balinya aliyekuwa mfungaji bora wa ligi kuu ya Uganda, awali alisajiliwa na Yanga kwa mkataba wa miaka miwili na kutambulishwa kwa mbwembwe wakati wa kilele cha siku ya wiki ya mwananchi jijini Dar es salaam.

banner

Hata hivyo alidumu Yanga kwa miezi sita tu, kabla ya makubaliano ya kuvunja mkataba baina yake na Yanga kufikiwa.

Nyota huyo ni kama amepishana na Yikpe Gnamien aliyesajiliwa na Yanga akitokea Gor Mahia.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited