Home Soka Bangala Atemwa Azam Fc

Bangala Atemwa Azam Fc

by Sports Leo
0 comments

Mabosi wa klabu ya Azam Fc wamefikia uamuzi wa kuachana na mchezaji kiraka Yanick Bangala kwa makubaliano ya pande zote mbili ili kupisha ingizo jipya kikosini humo.

Bangala aliyesajiliwa kwa mkataba wa miaka miwili baada ya kununuliwa chini ya kocha Yousouph Dabo kutoka Yanga sc amekubaliana na mabosi wa klabu hiyo kuvunja mkataba wake wa miezi nane uliosalia.

Mabosi wa Azam Fc ili kuepuka kufungiwa na Fifa kuhusu masuala ya usajili wameamua kumlipa mshahara yake yote iliyosalia kama gharama ya kuvunja mkataba huo ambapo sasa nafasi yake itachukuliwa na mshambuliaji Allasane Diao aliyekua majeruhi.

banner

Kocha Rachid Taoussi ameonekana kukubaliana na kiwango cha Allasane Diao na kuamuru arudishwe kwenye mfumo wa usajili klabuni hapo na beki huyo kuondolewa rasmi.

Tayari mchezaji huyo ameshapokea rasmi taarifa hiyo na sasa anaaglngalia ofa zingine ndani na nje ya Tanzania.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited