Home Makala Bao la Sakho Latinga Caf

Bao la Sakho Latinga Caf

by Dennis Msotwa
0 comments

Shirikisho la Soka Afrika limetangaza bao lililofungwa na Pape Sakho wa Simba kwenye mechi dhidi ya Asec Mimosas kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar es salaam  kuwa bao bora la wiki katika mechi za raundi ya kwanza hatua ya makundi Kombe la Shirikisho Afrika.

Sakho alifunga bao hilo dakika ya 12 ya mchezo huo wa kwanza kwa Simba sc hatua ya makundi ya kombe la shirikisho akipokea pasi ya upendo kutoka kwa Shomari Kapombe na kufunga kwa Tiktak akiruka kupiga mpira kuelekea nyuma na kufunga katika mchezo ulioisha kwa Simba sc kushinda 3-1.

Sakho aliyesajiliwa kutoka klabu ya Teungueth Fc inayoshiriki ligi kuu nchini Senegal amekua na kiwango cha kupanda na kushuka tangu ajiunge na ligi kuu nchini huku majeraha yakiwa yanamuandama mara kwa mara na kumfanya awe na kiwango imara.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited