Ni sawa na kusema kuwa Barcelona hawana kabisa na wala hawawazi kumuuza kinda wao Pedri kwa kuweka kipengele cha kumuuza(release clause) chenye thamani ya Paundi Bilioni moja za Kiingereza kwa klabu itakayotaka kupata saini ya kiungo huyo siku za usoni.
Kiungo huyo mwenye miaka 19 zao la akademi ya soka ya klabu hiyo La Masia amekuwa kwenye kiwango bora na kuwashangaza wapenzi wa soka duniani tangu alipopandishwa kikosi cha wakubwa msimu uliopita na kocha mkuu Ronald Koeman.
Pedri aliitwa na kuichezea timu ya Taifa ya Hispania katika michuano ya Euro 2020 ambapo alicheza mechi zote hadi hatua ya nusu fainali walipotolewa na Italia kwa mikwaju ya penati,baada ya michuano hiyo aliitwa tena kwenye kikosi cha Hispania kilichoshiriki michuano ya Olimpiki nchini Japan walipofungwa fainali na Brazil.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Barcelona wameweka kipengele hicho baada ya Pedri kusaini mkataba mpya wa miaka mitano wakimuona kama almasi na taswira ya timu hapo baadae hivyo hawataki kumpoteza.