Home Makala Barcelona Apokea Kichapo Cha Mabao 3-1

Barcelona Apokea Kichapo Cha Mabao 3-1

by Dennis Msotwa
0 comments

Barcelona imekubali kipigo cha mabao 3-1 mbele ya Real madrid katika mchezo wa Laliga uliochezwa leo majira ya saa 10:00 jioni katika uwanja wao wa nyumbani wa Camp Nou.

Real Madrid walianza kupachika bao la kwanza dakika ya 5 kupitia Federico Valverde ambapo lilisawazishwa na Ansu Fati wa Barcelona dakika ya 8.

Bao la pili la Real Madrid lilipachikwa na Sergio Ramos dakika ya 63 huku dakika ya 90 kabla ya kipenga cha kumaliza mchezo kupulizwa Luka Modric alipachika bao la tatu la ushindi kwa klabu yake.

banner

Real madrid wanabaki kileleni katika msimamo wa Laliga wakiwa nafasi ya kwanza na pointi 13 kibindoni katika miichezo sita waliyocheza.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited