Barcelona imekubali kipigo cha mabao 3-1 mbele ya Real madrid katika mchezo wa Laliga uliochezwa leo majira ya saa 10:00 jioni katika uwanja wao wa nyumbani wa Camp Nou.
Real Madrid walianza kupachika bao la kwanza dakika ya 5 kupitia Federico Valverde ambapo lilisawazishwa na Ansu Fati wa Barcelona dakika ya 8.
Bao la pili la Real Madrid lilipachikwa na Sergio Ramos dakika ya 63 huku dakika ya 90 kabla ya kipenga cha kumaliza mchezo kupulizwa Luka Modric alipachika bao la tatu la ushindi kwa klabu yake.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Real madrid wanabaki kileleni katika msimamo wa Laliga wakiwa nafasi ya kwanza na pointi 13 kibindoni katika miichezo sita waliyocheza.