Lusajo Mwaikenda ambaye ni beki chipukizi wa Azam Fc amesaini upya mkataba wake ambapo ataendelea kutumikia kikosi chake kwa miaka mitatu mbeleni.
Mkataba wa Lusajo ulitakiwa kumeguka mwezi Septemba mwaka huu lakini baada ya kukubali kusaini dili hilo atabaki ndani ya Azam Fc mpaka mwaka 2023.
Nyota huyo kwa sasa anacheza timu ya wakubwa inayoshiriki ligi kuu Tanzania Bara baada ya kupandishwa na timu hiyo msimu wa 2019/20.