Klabu ya Chelsea imelikosa kombe la Fa baada ya kufungwa kwa penati na Liverpool Fc katika mchezo wa fainali uliofanyika katika dimba la Wembley nchini Uingereza.
Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika timu hizo zilikua suluhu pamoja na dakika 30 za nyongeza pia hakuna timu iliyopata goli hali iliyomlazimu mwamuzi kuamuru mapigo ya penati ambapo Liverpool walishinda kwa penati 6-5 za Chelsea huku ikiwa zimepita siku 76 tu tangu Chelsea wafungwe katika michuano ya kombe la Carabao na kupelekea nafasi kwa Liverpool kuchukua makombe manne msimu huu.
Eduard Mendy alifanikiwa kumzuia Sadio Mane asiipe ushindi Liverpool baada ya kupangua penati yake lakini umakini wa Kipa Allison Becker aliyecheza penati ya Mason Mount iliyowarudisha mchezoni Liverpool na Kostas Tsimikas alifunga penati ya ushindi kwa Liverpool na kufikisha makombe mawili msimu huu ambayo yote wameyapata kwa kumfunga Chelsea fainali.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.