Home Makala David Kissu Aweka Rekodi

David Kissu Aweka Rekodi

by Sports Leo
0 comments

Kipa namba moja wa Azam FC,David Kissu ameweka rekodi ya kuwa kipa pekee ligi kuu bara baada ya kucheza dakika 360 sawa na mechi nne bila kuruhusu bao lolote.

Kissu alijiunga na Azam FC, akitokea Gor Mahia ya Kenya alipokipiga kwa mafanikio makubwa akifanikiwa kutwaa ubingwa wa ligi kuu nchini Kenya mara mbili.

Kisu amekusanya ‘clean sheet’ hizo kwenye mechi dhidi ya Polisi Tanzania, Coastal Union, Mbeya City na Tanzania Prisons ambapo amecheza kwa dakika 90 kwenye mechi zote.

banner

Azam Fc inashika nafasi ya kwanza ligi kuu bara ikikusanya jumla ya pointi 12, kwenye mechi nne walizoshuka dimbani huku wakifunga jumla ya mabao matano na wakiwa hawajaruhusu bao lolote hadi sasa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited