Msanii mkubwa wa kitaifa na kimataifa,Nasib Abdul alimaarufu kama Diamond Platnum ametua Uwanja wa Mkapa siku ya Simba Day na Helikopta na kuwateka mashabiki wote wa Simba kwa kutumbuiza.
Ni miaka 11 sasa tangu ianzishwe Simba Day chini ya aliyekuwa mwenyekiti wa klabu hiyo,Hassan Dalali.
Diamond Platnum ni kipenzi cha watanzania wengi nchini Tanzania na nje hivyo klabu hiyo imeamua kumualika msanii huyo kutumbuiza katika siku yao na kuwaburudisha mashabiki ambao wamefika Simba Day kabla ya kushuhudia mechi kali ya timu yao dhidi ya Vital’O’.
Â