Home Makala Domayo Nje kwa Majeraha

Domayo Nje kwa Majeraha

by Sports Leo
0 comments

Kiungo wa Azam FC, Frank Domayo, anatarajiwa kuwa nje ya uwanja kwa takribani mwezi mmoja kutokana na kusumbuliwa na majeraha ya mguu.

Domayo aliumia mguu kwenye mchezo wa kirafiki dhidi ya TP Mazembe uliochezwa hivi karibuni na kumalizika kwa sare ya 1-1 uliofanyika katika uwanja wa Chamazi Complex


Akizungumza na Sportsleobongo, Afisa Habari wa Azam FC, Thabiti Zakaria, amesema: “Domayo atakaa nje kwa muda wa mwezi mmoja kwa majeraha ya mguu aliyoyapata kwenye mchezo wetu na TP Mazembe.”

Huyu ni kati ya wachezaji mahiri kwenye kikosi cha Azam kutokana na jinsi ambavyo amekuwa akiitumikia timu hiyo uwanjani tangu ajiunge nayo mwaka 2014 akitokea kunako klabu ya Yanga sc.
.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited