Home Makala Hajji Arejea Mbao Fc Kama Kocha Mkuu

Hajji Arejea Mbao Fc Kama Kocha Mkuu

by Sports Leo
0 comments

Aliyekuwa kocha msaidizi wa Mbao Fc ,Abdulmutik Hajji amepewa nafasi na bodi ya Mbao Fc kuinoa timu hiyo kama kocha mkuu ili kusaidia kikosi hicho kufikia malengo hasa katika msimu huu wa ligi kuu.

Hapo awali kocha Hajji ambaye alikuwa msaidizi na bosi wake Hemedd Morroco wote waliamua kuondoka katika kikosi hicho kutokana na ubovu wa timu hiyo na madai ya kutokulipwa stahiki zao kama walivyokubaliana.

Mbao kwa sasa ipo nafasi ya 18 ikiwa na pointi 22 imecheza mechi 23 imeshinda mechi tano kazi yake kubwa  ya Hajji itakuwa ni kuinusuru timu hiyo kushuka daraja kutokana na nafasi iliyopo kwa sasa.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited