Home Makala Hatimaye Kane Atwaa Taji

Hatimaye Kane Atwaa Taji

by Dennis Msotwa
0 comments

Hatimaye mshambuliaji Harry Kane ametwaa kombe lake la kwanza kwenye maisha yake ya soka baada ya Bayern Munich kutwaa ubingwa wa Bundesliga baada ya Bayer Leverkusen kulazimishwa sare ya 2-2 dhidi ya Freiburg zikiwa zimesalia mechi mbili pazia la ligi kuu ya  Bundesliga kufungwa.

Bayern Munich ni Mabingwa wapya wa Bundesliga kwa kuwa pointi 76 walizonazo haziwezi kufikiwa na timu yoyote ambapo hata kama Leverkusen watashinda mechi zao mbili zilizosalia hawawezi kuzifikia pointi za Bayern.

Ikimbukwe kuwa mshambuliaji huyo kiongozi wa timu ya Taifa ya Uingereza hajawahi kutwaa kombe lolote katika ngazi ya klabu tangu awe mchezaji rasmi wa kulipwa.

banner

Kane kabla ya kujiunga na Bayern Munich ameichezea klabu ya Tottenham Fc kwa takribani miaka 11 ambapo hakutwaa taji lolote mpaka anajiunga na Bayern ambapo sasa ametwaa taji kwa mara ya kwanza.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited