Bayern Munich imenyooshwa kwa kuchapwa mabao 4-1 mbele ya Hoffenheim kwenye mchezo wa Bundesliga uliochezwa jana kwenye uwanja wa Rhein-Neckar.
Mabao ya Hoffenheim yalipachikwa na Ermin Bicakcic dakika 16, Mu’nas Dabbur dakika ya 24 na Andrej Kramaric alipachika mabao mawili dakika ya 77 na 90+2 kwa mkwaju wa penalti.
Munich walipachika bao kupitia Joshua Kimmich dakika ya 36 huku wakiondoka baada ya dakika 90 kukamilika wakiwa kama wamemwagiwa maji.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Mara ya mwisho Bayern Munich kupoteza mchezo ndani ya dakika 90 ilikuwa ni Januari 11 mwaka huu ambapo ilichapwa mabao 5-2 kwenye mchezo wa kirafiki dhidi ya Numberg.