Klabu ya Kaizer Chief ya Afrika Kusini Imefungua mlango wa mazungumzo na Uongozi wa klabu ya Yanga sc ya Tanzania kuona kama wanaweza kumpata Mlinda lango huyo bora kwenye dirisha kubwa la usajili.
Kocha Nasredine Mohamed Nabi anataka kuhakikisha kuwa kikosi chake kinapambana kumpata golikipa huyo mzoefu wa soka barani Afrika ambapo mpaka sasa Pamoja na klabu hiyo kutuma ofa bado haijajibiwa na klabu yake ya Yanga Sc.
Diarra mwishoni mwa msimu uliopita aliongeza mkataba wa miaka mitatu na klabu yake ya Yanga sc kuendelea kuitumikia klabu hiyo hivyo Kaizer Chiefs inapaswa kutoa fedha ndefu kumnasa kipa huyo aliyetokea kuwa kipenzi cha mashabiki wa klabu hiyo.