Home Makala Kally Apitiwa na Fagio Azam Fc

Kally Apitiwa na Fagio Azam Fc

by Sports Leo
0 comments

Kocha Kally Ongara ameungana na mastaa Cleophas Mkandala na Ismail Aziz Kader katika orodha mpya ya mastaa waliotupiwa virago na klabu hiyo ikiwa katika muendelezo wa kujijenga upya kwa ajili ya msimu ujao wa ligi kuu na michuano ya kimataifa.

Kally aliyekua kocha wa timu hiyo lakini kutokana na kutokua na vigezo timu ilikabidhiwa kwa kocha wa makipa Dani Cardena huku Kally akishikilia majukumu yote ya ufundi kwa ujumla japo awali aliajiriwa kama kocha wa washambuliaji.

Pia wachezaji Mkandala na Kader wametemwa kutokana na mapendekezo ya benchi la ufundi chini ya mwalimu mpya wa klabu hiyo Youssouph Dabo ambaye ndie anahusika na masuala ya usajili klabuni hapo kwa sasa.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited