Uongozi wa Mwadui FC umefikia maamuzi hayo baada ya Jumamosi kufungwa 5-0 na Yanga SC ukiwa mwendelezo wa vichapo vya goli nyingi katika ligi kwa msimu huu wa 2020-21.
Mwadui ilifungwa 6-1 na JKT pia Simba SC waliwachakaza 5-0 uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam na katika mchezo wa juzi Yanga nao waliwafunga mabao 5-0 ukiwa na ushindi wa kwanza mnono kwao.
Ushindi wa 5-0 ugenini dhidi ya Mwadui FC umepelekea klabu hiyo kumtimua kocha wake Khalid Adamu.