Kai Havertz ambaye ni kiungo mpya wa Chelsea ameeleza sababu kubwa iliyomfanya asaini ndani ya klabu hiyo ni kutokana na kuvutiwa na kocha mkuu wa timu hiyo, Frank Lampard kwani anampenda na anamfuatilia sana kocha huyo.
Harvest amesaini dili la miaka mitano ndani ya Chelsea inayoshiriki ligi kuu England akitokea Bayer Leverkusen inayoshiriki Bundesliga kwa dau la thamani ya pauni 72 milioni.
Nyota huyo anatimiza idadi ya wachezaji sita ambao tayari wameshamalizana na Chelsea ikiwa ni pamoja na Timo Werner, Hakimi Ziyech,Malang Sarr,Thiago Silva na Ben Chilwell.