Home Makala Kocha Ndanda Aingiwa Na Wasiwasi

Kocha Ndanda Aingiwa Na Wasiwasi

by Sports Leo
0 comments

Abdul Mingange ambaye ni kocha mkuu wa Ndanda FC amesema kuwa kusimamishwa kwa ligi kuu bara kwa muda wa mwezi mmoja kutawatoa wachezaji wake kwenye reli kutokana na kasi waliyoanza kuitengeneza.

Kikosi hiko kilikuwa kimerejea kwenye ubora wake ambapo kwa mwezi Februari Mingange aliingia kwenye kuwania tuzo ya kocha bora wa mwezi huku mchezaji wake Vitalis Mayanga akiibuka mchezaji bora wa mwezi Februari.

Mingange amesema kuwa kusimamishwa kwa ligi kwa sababu ya kupambana na Virusi vya Corona ni jambo la msingi kutokana na umuhimu wa afya lakini ana wasiwasi mkubwa na vijana wake kutoweza kurejea kwenye kasi ambayo walianza kuwa nayo.

banner

Ndanda Fc inashika nafasi ya 15 katika msimamo wa ligi kuu ikiwa na pointi 31 katika mechi 29 alizocheza huku akitoa sare 10 na kushinda mechi 7 huku akipoteza mechi 12.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited