Tetesi zinaeleza kuwa kiungo wa zamani wa klabu ya Simba,James Kotei amesaini kandarasi ya miaka miwili ndani ya klabu ya Yanga akiwa kama chaguo la kocha mkuu wa Yanga,Eymael ili kuboresha kikosi chake kwakuwa mchezaji huyo ana uzoefu kwenye ligi ya Bongo.
James Kotei baada ya kumaliza mkataba wake na Simba Sc alijiunga na klabu ya Kaizer Chief ya Afrika Kusini ila kwa sasa anakipiga ndani ya klabu ya FC Slavia-Mozŕy.
Ofisa Uhamasishaji na Msemaji mkuu wa Yanga,Antonio Nugaz amesema kuwa hawezi kuzungumzia suala hilo kwa kuwa wakati wa usajili haujafika.