Home Makala Ligi Kuu Bara Mchaka Mchaka

Ligi Kuu Bara Mchaka Mchaka

by Sports Leo
0 comments

Ligi kuu ya soka Tanzania bara inaendelea tena jioni ya leo kwa michezo mbalimbali ambayo itafanyika katika viwanja tofautitofauti nchini.

Singida United watawakaribisha Alliance mchezo utakaofanyika katika uwanja wa Namfua huku wakikumbuka sare waliyoipata dhidi ya mbao fc uwanjani hapo katika mchezo uliopita ambapo safu ya ushambuliaji wa klabu hiyo ilishindwa kubadili matokeo kutokana na kukosa nafasi za wazi.

Mbao watasafiri mpaka mjini Shinyanga kuwafata Mwadui huku wakikumbuka sare waliyoipata dhidi ya Singida united ugenini hivyo leo hawana budi kutafuta ushindi mbele wa Mwadui mchezo utakaofanyika katika uwanja wa Mwadui complex.

banner

Selemani Matola ataiongoza Polisi Tanzania kucheza ugenini dhidi ya Ruvu Shooting mchezo utakaofanyika katika uwanja wa mabatini ambapo Ruvu wanakumbuka kulazimishwa sare na Coastal union uwanjani hapo wiki iliyoisha.

Simba sc imesimama kileleni mwa msimamo wa ligi ikiwa na pointi 9 baada ya kushinda michezo mitatu iliyocheza mpaka sasa huku kagera wakiwa nafasi ya pili wakifanana pointi na Simba lakini wakiwa na wastani tofauti ya mabao ya kushinda na kufungwa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited