Home Makala Makonda Atimiza Ahadi

Makonda Atimiza Ahadi

by admin
0 comments

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda ametimiza ahadi aliyoiahidi ya kumzawadia shilingi milioni 10 kipa wa taifa stars Juma Kaseja kufuatia kiwango bora alichokionyesha dhidi ya Burundi na kuihakikishia ushindi kwa taifa stars.

Kaseja aliyeibuka mchezaji bora wa mechi hiyo aliahidwa kiasi hicho cha fedha na makonda kama sehemu ya motisha kwa wachezaji hao wa timu ya taifa na leo  fedha hizo amekabidhiwa rasmi mbele ya kocha wa Taifa stars,Katibu mkuu wa Tff na wachezaji kadhaa waliomsindikiza.

Kaseja amemshukuru makonda kwa kujitoa kwake baada ya kutimiza ahadi kwa muda mfupi huku akisisitiza pesa hiyo ni muhimu na itamsaidia katika kupambana na maisha.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited