Home Makala Mashabiki Uingereza Kurejea Uwanjani

Mashabiki Uingereza Kurejea Uwanjani

by Dennis Msotwa
0 comments

Taarifa zinaeleza kuwa huenda mashabiki wa soka nchini Uingereza wanaweza kurejea tena viwanjani hivi karibuni baada ya mashabiki hao kutoa ombi lililopata saini nyingi bungeni hapo na kupangwa kujadiliwa Novemba 9,mwaka huu.

Serikali ya nchini Uingereza ilipiga marufuku mashabiki kuinga viwanjani tangu mwezi Machi ambapo janga la Corona liliikuta Dunia,hivyo endapo ombi la mashabiki hao likifikiwa muafaka bungeni italeta unafuu kwa vilabu vingi ambavyo vinategemea zaidi mapato ya mlangoni.

Ligi nchini humo imekuwa ikiendelea na mpaka sasa ni raundi ya nne,licha ya kuwa hakuna amshaamsha ya uwanjani ya kuwapa motisha wachezaji.

banner

Msimamo wa ligi kuu Uingereza unaongozwa na Everton ambao wana pointi 12 wakiwa wameshinda michezo yote minne.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited