Home Makala Mbao Yaifunga Polisi Tz

Mbao Yaifunga Polisi Tz

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Mbao fc imeibuka na ushindi kiduchu wa bao 1-o dhidi ya polisi Tanzania mchezo wa ligi kuu Tanzania bara uliochezwa katika uwanja wa Ccm Kirumba.

Bao la mbao lilifungwa na Waziri Junior dakika ya 65 na lilidumu mpaka mwisho mwa mchezo na kuifanya Mbao fc kuchukua pointi 3 muhimu japo hazikutosha kuinyanyua katika msimamo wa ligi kuu ambapo imesalia nafasi ya 19 ikiwa na pointi 29 katika michezo 32.

Huu ni mchezo wa pili mfululizo kwa mbao kuibuka na ushindi chini ya kocha Felix Minziro ambapo awali waliifunga Coastal Union bao 1-0.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited