Aston Villa wamefanikiwa kumsajili Mbwana Samatta kwa mkataba wa miaka minne na nusu ambapo ataitumikia klabu hiyo hadi mwezi Juni 2024 kwa ada ya pauni milioni 8.5
Mbwana Samatta atakuwa na kibarua kuelekea kampeni ya ligi kuu na michuano mingine kuanzia wikiendi hii ambapo katika mechi 10 za kwanza Aston Villa itacheza na Watford (H), Leicester City (H), Bournemouth (A), Tottenham Hotspurs (H), Southampton (A), Sheffield United (H), Chelsea (H), Newcastle United (A), Wolverhampton (A), Liverpool (A).