Carlo Ancelotti amekuwa meneja wa kwanza kuonyeshwa kadi nyekundu katika ligi kuu England msimu huu kwenye mchezo uliowakutanisha Everton dhidi ya Man UTD kwenye uwanja wa Goodson Park siku chache nyuma.
Meneja huyo wa Everton akitokea Italia alipewa adhabu hiyo na mwamuzi wa mchezo Chris Kavanagh kwa kosa la kupinga maamuzi ya kukataliwa kwa bao lililofungwa na Dominic Calvert Lewin dakika za lala salama kabla ya kubainika lilikuwa offside .
Everton inashika nafasi ya 11 kwenye msimamo wa ligi kuu England ikiwa na pointi 37 katika mechi 28 alizocheza.