Klabu ya soka ya Barcelona imetangaza rasmi kuwa mshambuliaji na nahodha wa timu hiyo na timu ya taifa ya Argentina Lionel Messi hatosalia tena kwenye klabu hiyo kutokana na vikwazo vya kiuchumi na kikanuni vya ligi hiyo.
Messi amekuwa mchezaji huru tanagu Julai mosi mwaka huu pindi mkataba wake ullipoisha.
Barcelona na Messi walishakubaliana maslahi na mkataba mpya na hata kufikia kupunguza mshahara wake kwa asilimia 50 lakini kanuni za La Liga ziliwataka kupunguza mishahara na kuuza baadhi ya wachezaji kuendana na kanuni zao.Pande zote mbili zimesikitishwa kutokana na kushindwa kutimiza matamanio yao ya kuendelea kufanya kazi pamoja.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Klabu hiyo imemshukuru Mchezaji huyo kuhudumu kwa miaka 21 na imemtakia kila la kheri katika maisha yake ya soka na binafsi.