Kocha wa zamani wa Tottenham Hotspur, Mauricio Pochettino anatamani kuona siku moja anarejea katika klabu ya Newell’s Old Boys akiwa na staa wa Barceona,Lionel Messi.
Kama ambavyo Messi ameanzia soka katika klabu ya Newell’s Old Boys, Pochettino ambaye ni raia wa Argentina naye aliwahi kuichezea klabu hiyo.
Matumaini ya Pochettiino ni kuona siku moja anarejea katika klabu ya Newell’s Old Boys , lakini pia anaamini kuwa Messi atacheza hata kombe la dunia lijalo.
“Messi atacheza kombe la dunia Qatar 2022 na atafanya vizuri bila kujali umri wake atapambana tu, unajua uwepo wake ndani ya timu ni kitu kikubwa sana ataipambania tu Argentina kwenye michuano hiyo”alisema Pochettino