Home Makala Messi huyoo PSG

Messi huyoo PSG

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji wa kimataifa wa Argentina Lionel Messi amekubali mkataba wa miaka miwili kujiunga na matajiri wa jiji la Paris PSG hadi mwaka 2023 huku kukiwa na kipengele cha kuongeza mwaka mmoja zaidi.

Messi ataweka kibindoni kiasi cha Euro milioni 35 kama mshahara na marupurupu kukipiga Parc De Prince.

Mshambuliaji wa Kibrazil Neymar ambaye ni rafiki mkubwa wa Messi amekuwa akisukuma sana dili hilo.PSG ni klabu pekee iliyowasiliana na Messi moja kwa moja tangu alhamisi klabu ya Barcelona ilipotangaza kuwa ataondoka Nou Camp na anatarjiwa kutangazwa rasmi kama mchezaji wa PSG ndani ya masaa machache yajayo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited