Home Makala Mo Dewji Ashindwa Kujizuia Kuhusu Wawa

Mo Dewji Ashindwa Kujizuia Kuhusu Wawa

by Sports Leo
0 comments

Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi Simba Sc,Mohammed Dewji ‘Mo Dewji’ ameamua kuziweka hisia zake wazi kuhusu beki mkongwe wa klabu hiyo Pascal Wawa kutokana na ubora wa kiwango chake ndani ya kikosi.

Wawa ambaye ni beki wa kati ameichezea Simba misimu miwili ambayo  imetwaa ubingwa mfululizo akiwa kwenye kiwango kizuri ingawa anaonekana kuwa mchezaji mkongwe wa soka.

Mo Dewji amemwaga sifa nyingi kuhusu beki huyo katika ukurasa wake wa Instagram akisema “Pascal Wawa juhudi na nidhamu vimeendelea kukufanya kuwa bora kadri muda unavyoenda, nafasi ya beki huambatana na lawama nyingi kuliko pongezi lakini haijawahi kukusumbua wala kukupotezea umakini uwanjani.

banner

“Nathamini mchango wako na nina imani utaendelea kuwa sehemu muhimu ya Simba kuweza kufikia malengo yetu msimu ujao! Good interview Pascal”aliongeza Mwekezaji huyo wa Simba Sc.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited