Wachezaji Jesus Moloko na Salum Abubakar wataukosa mchezo wa leo dhidi ya Real Bamako ya nchini Mali utakaofanyika katika uwanja wa Benjamini Mkapa kutokana na sababu mbalimbali kwa mujibu wa kocha wa timu hiyo Nasredine Nabi.
Kocha huyo alisema kuwa Sure Boy amefiwa na mtoto wake wa kiume aitwaye Feisal Salum Abubakari ambaye tayari amezikwa jana jioni huku Jesus Moloko akisumbuliwa na maumivu ya mguu baada ya kuumia katika mchezo dhidi ya Tanzania Prisons ambao ulifanyika katika uwanja wa Chamazi Complex na Yanga sc kuibuka na ushindi wa mabao 4-1.
“Moloko bado hajawa imara ripoti yake ya mazoezi ya mwisho itaamua kama ataanza kikosi cha kwanza ama la lakini ukweli ni kuwa alipata maumivu.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
“Wengine ni wale wenye matatizo ya kifamilia lakini tupo tayari kupambana kupata matokeo,”.Alisema Nabi ambaye taarifa zinasema kwamba tayari ana ofa kadhaa za baadhi ya timu kubwa barani Afrika ikiwemo Tp Mazembe ya nchini Congo Drc.