Home Makala Morisson aishida Yanga CAS

Morisson aishida Yanga CAS

by Sports Leo
0 comments

Mahakama ya usuluhishi wa michezo duniani(CAS) imetupilia mbali rufaa ya kesi ya kimkataba kati ya klabu ya Yanga na mchezaji wa klabu ya Simba Benard Morisson katika hukumu iliyotoka hii leo.

Yanga waliamua kukata rufaa CAS baada ya kutoridhishwa na maamuzi ya kamati ya sheria na hadhi za wachezaji mwaka 202o ambapo pia Morisson alishinda.

Klabu hiyo ilikua inataka kurudishiwa zaidi ya milioni 460 za usajili na mchezaji huyo kwa kile walichodai kuwa mchezaji huyo amekiuka mkataba kwa kusaini Simba huku akiwa bado ana mkataba na Yanga.

banner

CAS imeiamuru klabu ya Yanga kulipa Tsh milioni 12 kama gharama za uendeshaji wa kesi hiyo.

Makamu mwenyekiti wa Yanga Fredrick Mwakalebela amesema kuwa wamkubali hukumu hiyo ya CAS kwa kusema imetokana na ushahidi wao kuonekana una mapungufu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited