Home Makala Morrison Aimaliza Dodoma Jiji Fc

Morrison Aimaliza Dodoma Jiji Fc

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Dodoma Jiji Fc huku Benard Morrison akipeleka mauaji katika mchezo huo uliofanyika katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.

Morrison alipiga krosi iliyounganishwa kwa kichwa na Meddie Kagere na kumshinda kipa Aron Kalambo na kuiandikia Simba sc bao la uongozi lililodumu kwa dakika 6 tu ambapo Cleofas Mkandala alisawazisha bao hilo kwa kichwa dakika ya 36 ambapo mpaka mapumziko mechi ilikua 1-1.

Kipindi cha pili dakika ya 67 pasi ya Perfect Chikwende ilimkuta Benard Morrison aliyepiga shuti kali lililozama wavuni na kuisaidia Simba sc kupata alama tatu katika mchezo huo mkali na wa kusisimua.

banner

Simba sc sasa imefikisha alama 38 katika msimamo ligi kuu huku ikiwa imecheza jumla ya michezo 16 ambapo imebakiza michezo miwili ili kumaliza viporo vya mzunguko wa kwanza.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited