Site icon Sports Leo

Mourinho Amtakia Eriksen Maisha Ya Furaha

WATFORD, ENGLAND - SEPTEMBER 18: Jose Mourinho, Manager of Manchester United takes a look around the pitch prior to kick off during the Premier League match between Watford and Manchester United at Vicarage Road on September 18, 2016 in Watford, England. (Photo by Richard Heathcote/Getty Images)

Kocha mkuu wa Tottenham Hotspur Jose Mourinho ameamua kumuaga mchezaji wake Christian Eriksen kwa kumtaka aondoke akiwa na furaha kwani mara kwa mara tetesi zilikuwa zikitajwa kuwa anataka kuondoka kwenye timu hiyo kwenye usajili wa Januari.

Christian Eriksen alionekana juzi akiwaaga wachezaji wenzake na mashabiki wa timu hiyo wakati Spurs ilipokuwa ikicheza na Middlesbrough kwenye mchezo wa kombe la FA pia kumpatia shabiki jezi yake aliyoitumia kwenye mchezo huo.

“Nafikiri anatakiwa kuondoka hapa akiwa na furaha ,ni mchezaji mkubwa ,mtiifu akiwa mazoezini pia amekuwa akionyesha kiwango cha juu sana kwenye kila mchezo”alisema Jose Mourinho.

Eriksen anatarajiwa kuondoka kwenye timu hiyo na kujiunga na Inter Milan kama iliyosemekana walikuwa wakimuhitaji mchezaji huyo.

Exit mobile version