Home Makala Mutale Arejea Chipolopolo

Mutale Arejea Chipolopolo

by Sports Leo
0 comments

Winga wa klabu ya Simba Sc Joshua Mutale ameitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Zambia (Chipolopolo) kwa ajili ya michezo ya kirafiki ya kalenda ya Fifa.

Mutale amerejea baada ya muda mrefu kukosekana kutokana na kutopata nafasi katika klabu yake ya Simba Sc na hivyo kukosa nafasi pia katika timu ya Taifa hilo.

Zambia itacheza na Sudan na Tunisia katika ratiba ya michezo ya kirafiki ya kalenda ya Fifa ambapo kocha Avram Grant ameita mastaa takribani 25 katika kikosi hicho.

banner

Mbali na Mutale pia mastaa wa Yanga Sc Kennedy Musonda na Clatous Chama nao wameitwa kwa ajili ya michezo ya kirafiki ya FIFA dhidi ya Sudan na Tunisia.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited