Home Makala Mvua Yasitisha Mechi Ya Kirafiki

Mvua Yasitisha Mechi Ya Kirafiki

by Sports Leo
0 comments

Kutokana na mvua kubwa kunyesha leo Jijini Dar-es-salaam,imepelekea mechi ya kirafiki ya Simba Sc dhidi ya Ndanda Fc kughairishwa.

Mechi hiyo ilitakiwa kuchezwa leo Octoba 13, majira ya saa 11:00 jioni uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi kwa dhumuni la kuviweka sawa vikosi hivyo katika michuano yao ijayo na timu zingine.

Simba Sc ambao ni mabingwa watetezi wa ligi kuu ,kwa sasa inashiriki ligi kuu bara msimu wa 2020/2021 huku Ndanda Fc iliyoshuka msimu uliopita wa 2018/2019 inashiriki ligi daraja la kwanza tayari kujiweka sawa kwa msimu ujao wa ligi.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited