Home Makala Ndala Akalia Kuti Kavu Azam Fc

Ndala Akalia Kuti Kavu Azam Fc

by Sports Leo
0 comments

Kiungo Issah Ndala anaweza kutemwa katika kikosi cha Azam Fc ili kumpisha kiungo Yannick Bangala ambaye amejiunga na timu hiyo akitokea klabu ya Yanga sc baada ya kukamilisha usajili mapema hivi leo.

Ndala inasemekana kuwa sio chaguo la kocha wa Azam Fc Yousouph Dabo na ndio maana aliwaruhusu viongozi kumsajili Bangala baada ya kumuona katika mchezo wa fainali ya kombe la shirikisho uliofanyika jijini Tanga mwezi juni mwaka huu.

Bangala ambaye ni mchezaji bora wa ligi kuu nchini msimu wa 2021/2022 alianza kuwekwa benchi na kocha Nasredine Nabi ambaye alianza kumtumia zaidi Khalid Aucho sehemu ya kiungo cha chini.

banner

Azam Fc ilimsajili Ndala baada ya kumuona katika mchezo wa michuano ya klabu bingwa barani Afrika dhidi ya Plateau Fc ya nchini Nigeria.

Azam Fc inalazimika kumchomoa Ndala katika usajili wao ili kutimiza idadi ya wachezaji 12 wa kigeni wanaotakiwa kwa mujibu wa kanuni za ligi kuu nchini.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited