Home Makala Nuno: Kane bado mchezaji wetu

Nuno: Kane bado mchezaji wetu

by Sports Leo
0 comments

Kocha wa klabu ya Tottenham Hotspurs Nuno Espirito Santo amesema kuwa nahodha ya timu hiyo Harry Kane bado ni mchezaji wao kwasasa na atamsubiri wazungumze atakaporejea.

Mchezaji huyo yupo katika mapumziko ya likizo baada ya kuiongoza England katika fainali za michuano ya Euro 2020.

Mchezaji huyo anaamini kuwa ana makubaliano ya mdomo ya  kiungwana na mtendaji wa timu hiyo Daniel Levy kuruhusiwa kuondoka na ameweka wazi nia yake ya kuondoka katoka dirisha hili, akihusishwa zaidi kuhamia kwa mabingwa wa England Manchester City.

banner

Nuno aliongeza ”ninamtakia mapumziko mazuri,ili atakaporejea aone ni jinsi gani  kila mmoja wetu anavyojitolea ilimtuwe bora.

”Sisi ni watu wenye ndoto na mipango thabiti,tunataka kufanya vema na tunamtegemea kwa sababu ni mchezaji bora wa daraja la dunia”.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited