Home Makala Nyota Ya Ninja Yang’aa Fk Rigas

Nyota Ya Ninja Yang’aa Fk Rigas

by Dennis Msotwa
0 comments

Beki wa kati wa Tanzania Abdallah Shaibu Ninja anatakiwa kutua nchini Latvia tarehe 15 ,Februari kwaajili ya kufanya vipimo katika klabu ya FK Rigas Footbola Scola inayoshiriki ligi kuu nchini humo na iwapo atafuzu atasaini mkataba usiopungua mwaka mmoja.

Kabla ya kuanza safari ya FK Rigas Footbola Scola ,Ninja alikuwa amesajiliwa timu ya MFK Vyskov ya jamhuri ya Zcech kwa miaka minne ila hakuweza kuitumikia timu hiyo kwani alichukuliwa kwa mkopo na timu inayoshiriki ligi kuu Marekani La Galaxy.

Mkurugenzi wa Ufundi wa Fk Rigas ,Aleksandrs Usovs  alituma kadi ya mualiko kwa mchezaji huyo na kumpa ofa ya kumgharamikia mahitaji yote muhimu atakayohitaji hadi ukamilisho wa vipimo utakapo kamilika.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited