Home Makala Ole Gunnar Akomaa Na Sancho

Ole Gunnar Akomaa Na Sancho

by Dennis Msotwa
0 comments

Miongoni mwa dili ambalo limezungumzwa kwa muda wote na halijaonesha mafanikio ndani ya Manchester united ni la Jadon Sancho ambaye ameifungia Borrusia Dortmund jumla ya mabao 20 msimu uliopita na kutoa pasi 20 kwenye mashindano yote.
Manchester United bado wana imani kuwa watamsajili Sancho ambaye ni chaguo la kwanza la kocha mkuu wa klabu hiyo,Ole Gunnar Solskajaer kabla ya dirisha la usajili kufungwa.
Kwa mujibu wa ripoti ya Dagbladet ,Solskjaer amemwambia nyota huyo wa Borussia Dortmund, Jadon Sancho kuwa dili lake la kujiunga na United litakamilika hivi karibuni.
Mpaka sasa United walishindwa kutoa fedha ya pauni milioni 108 ambayo Dortumund wanahitaji ili wamuachie kiungo Sancho mwenye uwezo mkubwa ndani ya uwanja.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited