Home Makala Pochettino Yu Huru Sasa

Pochettino Yu Huru Sasa

by Sports Leo
0 comments

Kocha wa Tottenham Hotspurs, Mauricio Pochettino sasa yuko huru kujiunga na klabu yoyote anayoitaka bila vikwazo kutoka kwa waajiri wake baada ya marufuku ya miezi sita yaliyomzuia kufanya hivyo kukamilika.

Tottenham ilizuia klabu yoyote kumnyakua kocha huyo kabla ya miezi sita kukamilika kwa kuweka sharti kuwa klabu inayomtaka lazima ilipe timu hiyo kutoka kaskazini mwa London milioni 34.6 ndipo imuajiri mwamba huyo kwa sababu ilikuwa imemlipa Pochettino fidia ya kumtema kabla ya kandarasi kumalizika.

Kukamilika kwa miezi hiyo kunamweka Pochettino huru kuchukuliwa na klabu yoyote bila ya ada kutolewa kwa mabosi wa Tottenham Hotspurs.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited