Home Makala Puto Lamponza Lacazette

Puto Lamponza Lacazette

by Dennis Msotwa
0 comments

Arsenal wamepanga kumwadhibu vikali mshambuliaji, Alexandre Lacazette baada ya kupata ripoti kuwa nyota huyo ambaye ni mzaliwa wa Ufaransa alipatikana akivuta gesi ya Nitrous Oxide maarufu kama ‘Laughing Gas’ iliyokuwa imejazwa ndani ya puto .

Gazeti la Daily Star nchini Uingereza lilichapishwa makala zenye picha zilizoonyesha Lacazette akiwa na puto yenye gesi hiyo mdomoni.

Ni wiki moja pekee imepita tangu Lacazette apatikane miongoni mwa wanasoka wengine wa Arsenal waliokiuka kanuni mpya za afya zinazodhibiti maambukizi dhidi ya virusi vya corona.

banner

Lacazette pia  alionekana akiwa karibu sana na mwanamume mmoja aliyekuwa akimwoshea gari lake jijini London, Uingereza na kuvunja kanuni inayotaka mtu kudumisha umbali wa hadi mita mbili kati yake na mwingine .

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited