Mabosi wa usajili wa klabu ya Manchester United wanaamini usajili wa Cristiano Ronaldo klabuni hapo utavutia mastaa wakubwa duniani kuja kujiunga na klabu hiyo ili wapate nafasi ya kucheza na staa huyo maarufu duniani.
Ronaldo 36 alijiunga na Manchester United mwishoni mwa dirisha la usajili akitokea Juventus kwa dau la Paundi milioni 28 na kuikacha klabu wapinzani Manchester City ambao walipewa kipaumbele kumsajili mreno huyo mwenye rokodi wa Guinnes ya kufunga mabao mengi katika timu ya Taifa akifunga mabao 111 mpaka sasa.
Mabosi hao bado wana nia ya kurudisha utawala wa Man united wa kuchukua makombe na kusajili mastaa ambapo hivi sasa wanapambana kumuongezea mkataba kiungo Paul Pogba huku pia wakiangalia uwezekano wa kumsajili Eerlin Haaland anayechezea Borrusia Dortmund wakiamini staa huyo atavutika kucheza na Ronaldo timu moja.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.