Home Soka Ronaldo Kumleta Haaland Old Trafford

Ronaldo Kumleta Haaland Old Trafford

by Dennis Msotwa
0 comments

Mabosi wa usajili wa klabu ya Manchester United wanaamini usajili wa Cristiano Ronaldo klabuni hapo utavutia mastaa wakubwa duniani kuja kujiunga na klabu hiyo ili wapate nafasi ya kucheza na staa huyo maarufu duniani.

Ronaldo 36 alijiunga na Manchester United mwishoni mwa dirisha la usajili akitokea Juventus kwa dau la Paundi milioni 28 na kuikacha klabu wapinzani Manchester City ambao walipewa kipaumbele kumsajili mreno huyo mwenye rokodi wa Guinnes ya kufunga mabao mengi katika timu ya Taifa akifunga mabao 111 mpaka sasa.

Mabosi hao bado wana nia ya kurudisha utawala wa Man united wa kuchukua makombe na kusajili mastaa ambapo hivi sasa wanapambana kumuongezea mkataba kiungo Paul Pogba huku pia wakiangalia uwezekano wa kumsajili Eerlin Haaland anayechezea Borrusia Dortmund wakiamini staa huyo atavutika kucheza na Ronaldo timu moja.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited