Mchezaji mpya wa Aston Villa aliyesajiliwa kwa dau la pauni milioni 8.5 akitokea KRC Genk Mbwana Ally Samatta ameanza mazoezi rasmi kwenye kikosi chake kipya.
Mbwana Samatta ameweka rekodi ya mtanzania wa kwanza kufanya kazi England kwenye timu inayoshiriki ligi kuu ambayo ni timu kubwa Uingereza Aston Villa.
Mtanzania mwingine aliyefanya majaribio mwanzoni mwa miaka ya 2020 ni Mrisho Ngasa katika kikosi cha West Ham United chini ya kocha Granfranco Zola lakini hakuweza kufanikiwa.