Home Makala Samatta Aanza Na 2-1 Fenerbahce

Samatta Aanza Na 2-1 Fenerbahce

by Sports Leo
0 comments

Nahodha wa Tanzania aliyejiunga na klabu ya Uturuki,Fenerbahce kwa mkopo akitokea Aston Villa,Mbwana Samatta ameanza kufanya yake kwa mara ya kwanza ndani ya klabu hiyo mpya kwa kupachika mabao 2-1 dhidi ya Faith Karagumruk kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Uturuki.
Licha ya kutumia dakika 84 uwanjani Sukru Saracoglu ,Samatta alitupia mabao hayo dakika ya 24 kwa pasi ya Caner Erkin huku bao la pili akilitupia dakika ya 68.
Nyota huyo mwenye miaka 27 ni mechi yake ya kwanza kuanza kikosi cha kwanza ambapo ile ya kwanza dhidi ya Galatasaray alianzia benchi na alicheza kwa dakika 25 na mechi kumalizika kwa suluhu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited