Home Makala Samatta Atoa Neno Kwa Watanzania

Samatta Atoa Neno Kwa Watanzania

by Dennis Msotwa
0 comments

Nyota mpya wa Aston Villa Mbwana Samatta amewashukuru  sana watanzania na watu wote waliokuwa wakimuombea mema aweze kupita katika usajili huo na ameahidi kuendelea kupambana kwani alipofikia ni suala la kumshukuru mungu.

Samatta mwenye miaka 27 alianza kucheza ndani ya Simba na kujinga Tp Mazembe aliibuka KRC Genk mwaka 2016 ambapo amefunga jumla ya mabao 76 kwenye mechi 191 ndani ya Genk na mabao 18 katika mechi 51 za timu ya Taifa ya Tanzania.

“Ninamshukuru Mungu kwa hatua niliyofikia kwa sasa ,sapoti ya mashabiki na maombi ya watanzania kiujumla yananifanya niwe hapa nilipo”alisema Samatta.

banner

Kutokana na utaratibu wa ligi kuu England kuwasilisha wachezaji kabla ya masaa 15 ya mchezo inamfanya Mbwana Samatta kutoweza kushiriki mechi ya leo dhidi ya Watford.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited